Samir Nasri ajiunga na Sevilla ya HIspania kwa mkopo toka Man City

Manchester City wamethibitisha kiungo mshambuliaji wao Samir Nasri kujiunga na Sevilla kwa mkopo wa msimu mzima.

Awali iliripotiwa kwamba, Nasri angejiunga na miamba ya Uturuki Besiktas, lakini mwishoni kabisa Sevilla wameonekana kuwa na mkono mrefu zaidi.

Mkurugenzi wa Ufundi wa Sevilla Monchi ametanabaisha kwamba, Nasri ni mchezaji ambaye wamekuwa wakimfukuzia kwa muda wote kwenye dirisha hili la usajili.

Mkataba huo wa mkopo hauna kipengelea cha Nasri kununuliwa moja kwa moja endapo Sevilla watahitaji kufanya hivyo.