Waziri mkuu Majaliwa atembelea eneo la Inyonga wilayani Mlele, Katavi

 Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akikagua ujenzi wa wodi katika zahanati ya Inyonga wilayani Mlele amabayo inatarajiwa kupandishwa hadhi na kuwa hospitali ya wilaya . Alikuwa katika ziara ya mkoa wa Katavi Agosti22, 2016.


 Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa na mkewe Mary wakiwapungia wananchi wa Inyonga baada ya waziri Mkuu kutawazwa kuwa Chief wa Wakonongo na kupewa jina la Chief Kayamba wa Kwanza katika mkutano wa hadhara uliofanyika kwenye uwanja wa Shule ya Msingi Inyonga Agosti 22, 2016. Kulia ni Cheif wa Wakonongo, Kayamba wa Pili.

 Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akiteta na Naibu Waziri wa Maji na Umwagiliaji ambaye pia ni Mbunge wa Katavi, Mhandisi Isaack Kamwelwe katika mkutano wa hadhara aliouhutubia kwenye uwanja wa shule ya msingi ya Inyonga wilayani Mlelele Agosti 22, 2016.

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akihutubia Mkutano wa hadhara kwenye uwanja wa Shule ya Msingi ya Inyonga wilayani Mlele Agosti 22, 2016.