Samatta apata leseni Belgium na kununua ndinga ya 130m

 Mshambuliaji wa kimataifa wa Tanzania anayekipiga katika klabu ya KRC Genk ya ligi kuu ya Belgium – Jupiter League – Mbwana Ally Samatta, jana kupitia akaunti ya Instagram ameonyesha ‘ndinga’ yake aliyoinunua baada ya kupata liseni ya kuendesha gari nchini Belgium.

Samatta ambaye alikuwa nje ya uwanja kwa wiki kadhaa baada ya kupata majeruhi, jana usiku alikuwemo katika katika kikosi cha Genk kilichoifunga Sassuolo 3-1 katika mchezo wa Europa League.

Gari alionunua Samatta ni Merecedez Benz Cla220 Cdi AMG Sport 2016 – ambayo imemgharimu kiasi cha €46,680 ambayo ukiizidisha kwa fedha za madafu inakuwa zadi ya millioni 130.

Inakadiriwa Mbwana Samatta ambaye ana mkataba na KRC Genk mpaka 2020, analipwa kiasi cha 35,600 kabla ya kodi kwa mwezi.