VIDEO: Walichokijibu CHADEMA kuhusu tuhuma za kuchochea mgogoro wa CUF

Wakati mgogoro wa chama cha wananchi CUF ukiendelea na huku ikielezwa moja ya chachu ya mgogoro huo ni kutoka chama cha demokrasia CHADEMA, leo September 30 2016 Mwenyekiti wa CHADEMA, Freeman Mbowe ammejibu tuhuma za kuwa CHADEMA imekuwa wakala wa mgogoro kwenye chama cha CUF, Mbowe amesema…….
Prof Lipumba ambaye mara kwa mara amesikika akisema kuwa CHADEMA ni wachochezi wakubwa na wanapandikiza mgogoro ndani ya CUF, sikusudii kumjadili Lipumba na nikiendelelea kumjadili nitampa nafasi aliyokuwa nayo zamani’

Sisi kama chama cha siasa tutaendelea kushirikiana na chama cha wananchi CUF, tutaendelea kuheshimu maamuzi yanayofanyika kwenye vikao halali  vya chama cha wanachi CUF, tutaendelea kufanya kazi na wabunge na madiwani wa UKAWA, tunaomba viongozi wote wa CHADEMA wapuuze na wasimpe ushirikiano wowote Prof. Lipumba’;-Mbowe