Vifaa Vya Sangoma Vyanaswa Uwanja Wa Taifa, Yanga, Simba Watupiana Mzigo

 Unaweza kusema utamu kunoga! Mechi ya watani, Yanga na Simba haikosi vituko.

Kuna taarifa kwamba kuna vitu vinavyoashiria hali ya kishirikina vimekamatwa kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam kabla ya mechi ya watani, Yanga na Simba, kesho.

Wakati vimekamatwa jana, lakini kila upande unatupa mpira kwa upande mwingine, kwamba ndiyo chanzo au unahusika.

Yanga wanasema ni Simba, nao Simba wanasema ni Yanga. Basi ili mradi siku zinasogea na inaendelea kuthibitika kwamba mechi hizo hasa za watani, watu ndiyo riziki zao.