Wema Sepetu awashukuru waliomtumia salamu za birthday

Jumatano hii ilikuwa ni siku ya kuzaliwa ya staa wa filamu Wema Sepetu ambao ndugu, jamaa pamoja na marafiki walimtakia heri na mafanikio mrembo huyo.

Moja kati ya vitu ambavyo vilileta gumzo kwenye mitandao ya kijamii ni baada ya mama Diamond kum-wish malkia huyo wa filamu huku akimkaushia Zari ambaye ni mama watoto wa Diamond.

Pia dada zake na Diamond walim-wish maklia huyo.

Baada ya kupokea salamu za watu mbalimbali kutoka katika kila kona ya dunia malkia huyo wa filamu na yeye aliamua kuwashurudu huku akionyesha kile ambacho hakukitarajia.

Wema kupitia istagram aliandika:
Wow… wow… wow… daah.. sijui cha kuandika.. am just out of words… Wema mimi nitamlipa nini Mungu kwa Neema na Baraka zake anazonijalia kila siku…?? Napenda kutoa shukrani zangu za Dhati kwa mumumu wangu, My family, my management, teamkazi wale kwa kufungua dimba last Night with that amazing suprise… alafu sasa huku insta, snapchat, twitter and kila site ambazo mmepost about My birthday nashindwa cha kusema.. toka nimeamka najitahidi kujibu kila post ninazoziona.. ila zinanielemea… ila ninajitahidi, nitajitahidi na nitahakikisha najibu Kila ambayo nakutana nayo… ila Daaah You Guys mnajua kupenda.. mpaka najiogopa kwa mapenzi mnayonipa.. what should i say?? Wakwe vepe?? Mawifi je?? Wake wenza nao ndani? Boyfriends🙈🙈 nacheka peke yangu….. And sometyms hadi machozi ya furaha yananitoka… Nimekuwa Cry baby wa kujitegemea tokea saa sita usiku…. Na nadhani zoezi litaendelea mpaka siku hii iishe…. Nawapenda jamani… #AmaBeBack