Ciara na Russell Wilson wanatarajia kupata mtoto wao wa kwanza

Ciara na mumewe Russell Wilson wanatarajia kupata mtoto wao wa kwanza – kwa mujibu wa mtandao wa E! News.

Mmoja wa watu wa karibu wa familia hiyo ameuambia mtandao huo kuwa Ciara ni mjamzito na anatarajia kuitwa mama tena hivi karibuni. “Ciara is pregnant and is so excited to be a mom. Russell Wilson would like to have two to three children. They both would like a big family,” kimesema chanzo hiko.

Huyo atakuwa ni mtoto wa kwanza kwa Russell na wa pili kwa Ciara baada ya mtoto wake wa kwanza Zahir Wilburn aliyezaa na ex wake, rapper Future miaka miwili iliyopita.

Wawili hao walifanikiwa kufunga ndoa mwezi Julai, mwaka huu mjini Liverpool.