Kufutia diwani machachari wa kata ya Tanga Songea mkoani Ruvuma kwa tiketi ya Chadema Bw.Mussa Ndomba kurudi CCM na kuwaacha wananchi wake njia panda bila uwakilishi,wananchi wake wamesikitikia hatua hiyo.
Wakati akirejesha kadi yake ya CHADEMA kwenye ofisi za CCM mkoa wa Ruvuma Bw.Mussa Ndomba ametaja sababu mbalimbali za kujitoa kwenye chama hicho ikiwemo kutishiwa maisha yake na makundi yanayopingana kwenye chama cha Demokrasia na maendeleo Ruvuma na kukiukwa kwa katiba ya CHADEMA katika kufanya maamuzi na uteuzi wa viti Maalum.
Wakati wana CCM wakifurahia hatua ya Bw.Mussa Ndomba kwenda CCM wakazi wa kata ya Tanga wamesikitishwa na hatua hiyo kwa kuwa watakosa uwakilishi kwa muda.
Akimpokea Bw.Ndomba Mwenyekiti wa CCM mkoa wa Ruvuma Bw Oddo Mwisho ameiomba serikali kumuhakikishia usalama wake.