Askari wa jeshi la zimamoto wakishirikiana na askari wa jeshi la polisi kuzima moto uliokuwa ukiunguza bweni la shule ya Ufundi Mtwara. Picha na Haika Kimaro
Katika tukio hilo lililotokea juzi saa moja asubuhi, hakuna aliyejeruhiwa kwa kuwa baadhi ya walimu kutoka shule mbalimbali mkoani hapa waliokuwa wakilitumia hawakuwamo ndani na wanafunzi wapo
likizo.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mtwara, Thobias Sedoyeka amesema hakuna madhara kwa binadamu na kueleza chanzo cha moto huo kinachunguzwa na taarifa zitakapokuwa tayari zitatolewa.
Mmoja wa walimu aliyekuwa katika semina shuleni hapo, Masele Francis amesema waliona moshi ukitoka katika bweni hilo na walipofuatilia waligundua kuwa kuna moto na kitu walichofanya ni kufuatilia kama kulikuwa na watu ndani ndipo walipobaini kwamba mwenzao mmoja alikuwa bafuni na kumuokoa.
