Hayo yameelezwa jijini Dar es Salaam na Mkurugenzi Mtendaji wa Tanesco Eng. Felchesmi Nramba mara baada ya kutembelea na kukagua hali ya miradi minne mikubwa inayotekelezwa hapa jijini kikiwemo kituo cha Muhimbili ambacho kitatumika maalum kwa hospitali ya Taifa Muhimbili na taasisi zake ili iondokane na kero ya umeme inayokabiliana nayo.
Kuhusu mradi wa kusambaza umeme mikoa zaidi ya kumi utakaoanzia mkoa wa Iringa hadi Mwanza Bw Mramba amesema umekamilika kwa asilimia 99 na unatarajiwa kufunguliwa na Rais Magufuli mwezi Januari mwaka huu.