Rais mpya wa Gambia Adama Barrow amerejelea ahadi yake aliyotoa wakati wa uchaguzi mkuu, kwamba taifa hilo halitajiondoa kutoka ndani ya mahakama ya kimataifa ya makosa ya jinai, (ICC), na kubadili uamuzi wa mtangulizi wake Yahya Jammeh, ambaye alikuwa anapinga mahakama hiyo, huku akiitaja kama "Mahakama ya kimataifa inayoendesha hukumu zake kwa misingi ya ubaguzi wa rangi, hasa ikiwahukumu tu waafrika".
Bw Barrow alisema hayo, baada ya kukutana kamishena wa tume ya ushiriikiano na maendeleo ya jumuia ya mataifa ya bara Ulaya, Neven Mimica, katika mji mkuu, Banjul.
Bw Mimica, alisifia tangazo hilo kwa kuandika kwwenye mtandao wake wa kijamii wa Twitter:
Bw Barrow alishinda uchaguzi mkuu wa Disemba 1, 2016, kwa ahadi ya kupigania haki za binadamu na uhuru, na kumaliza unyanyasaji ambao raia wa Gambia wamepitia wakati wa utawala wa miaka 22 wa Bw Jammeh.
Naye mwaandishi mmoja wa habari wa Uingereza nchini Gambia, ameandika katika mtandao wake wa Twitter kuwa Jumuia ya bara Ulaya, imeahidi kuzidisha mara dufu msaada wake kwa taifa hilo dogo la Afrika Magharibi:
Bw Barrow alisema hayo, baada ya kukutana kamishena wa tume ya ushiriikiano na maendeleo ya jumuia ya mataifa ya bara Ulaya, Neven Mimica, katika mji mkuu, Banjul.
Bw Mimica, alisifia tangazo hilo kwa kuandika kwwenye mtandao wake wa kijamii wa Twitter:
Bw Barrow alishinda uchaguzi mkuu wa Disemba 1, 2016, kwa ahadi ya kupigania haki za binadamu na uhuru, na kumaliza unyanyasaji ambao raia wa Gambia wamepitia wakati wa utawala wa miaka 22 wa Bw Jammeh.
Naye mwaandishi mmoja wa habari wa Uingereza nchini Gambia, ameandika katika mtandao wake wa Twitter kuwa Jumuia ya bara Ulaya, imeahidi kuzidisha mara dufu msaada wake kwa taifa hilo dogo la Afrika Magharibi:


