Wachezaji wa Manchester City wakimpongeza David Silva baada ya kufunga bao la kwanza dakika ya tatu Uwanja wa Riverside usiku wa jana katika mchezo wa Robo Fainali Kombe la FA England dhidi ya wenyeji, Middlesbrough. Man City ilishinda 2-0, bao lingine likifungwa na Sergio Aguero dakika ya 67.