Man U, Real Madrid, Chelsea zamuwinda Mbappe

London, England. Kinda wa Monaco sasa amewaingiza makocha wa timu  mbalimbali kwenye hekaheka ya kusaka saini yake kutokana kuimarisha kiwango chake cha soka akiwa uwanjani.

Nyota huyo kijana, wiki amekuwa gumzo kutokana na timu mbalimbali kuonyesha nia ya kumsajili wakati wa madirisha ya usajili yatakapofunguliwa kwa kila nchi husika.

Nahodha wa Ufaransa, Hugo Lloris amesema mchezaji huyo anaweza kuwa miongoni mwa wachezaji wakali iwapo ataendelea na kasi yake aliyoionyesha.

Juzi, Rais wa Real Madrid alionyesha nia yake ya kumsajili ili kumleta kikosini hapo kwa lengo la kumuongezea makali Karim Benzema.

Mbappe mwenye miaka 18 ameshafunga mabao 19 katika mashindano yote aliyoichezea Manaco huku pia akitajwa kuondoka klabuni hapo siku zijazo.
Mpya zaidi Nzee zaidi

Popular Items