Mbinu za Kutunza Ngozi yenye Mafuta

Sababu ya ngozi kuwa na mafuta hutokana na  na tezi za sebaceous na kuzalisha mafuta zaidi ya kiwango ambacho ambacho kinatakiwa. Lakini licha ya tezi hizo aina za sebaceous kuzalisha kiwango cha mafuta kwa wingi, zipo pia sababu nyingine ambazo zinafanya ngozi kuwa na mafuta ambazo kama ifuatavyo.

  1. • Kurithi.
  2. • Lishe.
  3. • Kiwango cha homoni mbalimbali mwilini.
  4. • Ujauzito.
  5. • Baadhi ya vipodozi .
  6. • mabadiliko ya hali ya hewa hasa joto.

Na madhara ambayo yanatokana na ngozi yenye mafuta ni kwamba, ngozi huweza kutengeneza ngozi yenye tabaka lisiloisha vipele pamoja na  chunusi kwa muda mrefu.

Baada ya kuona baadhi ya sababu na athari ya ngozi kuwa mafuta,  sasa tuangalie namna ya kutunza ngozi zenye mafuta:

1. Ngozi yenye mafuta inahitajia kusafishwa vyema kwa maji ya moto na sabuni ili kuzuia vinyweleo visizibwe na mafuta. Lakini Jitahidi kuitunza vyema ngozi yako na kuisafisha vizuri. Jaribu kuosha uso mara mbili au mara tatu kwa siku. Usioshe mara nyingi kwani kufanya hivyo huufanya uso kutoa mafuta zaidi.

3. Epuka kutumia vipodozi ambavyo huifanya ngozi yako ipoteze maji au kukauka. Kwani husababisha sehemu ya juu ya ngozi inyauke, na hivyo kusababisha mafuta kuziba vinyweleo na kupelekea kutokea kwa chunusi ambazo zitaufanya mwili kuwa na mafuta.

4. Chagua kile unachosafishia kwa makini, jiepushe kutumia cream nzito nzito au vifaa vugumu wakati wa kuosha uso wako. Ni bora utumie sabuni za kawaida zisizokuwa na madawa. Unaweza kutumia lotion ya kuua bacteria au sabuni zisizo na dawa nyingi (lightly medicated), au sabuni zenye madini mbalimbali. Ni bora usioshe au kutumia lotion au michanganyiko yenye alkoholi.

5. Lakini pia unashauriwa ya kwamba hakikisha unatumia  mafuta ambayo  yametengenezwa kwa ajili ya ngozi yenye mafuta.

Endapo utayazingatia hayo mwili wako utakwenda kuwa katika hali ya ubora zaidi, na kufurahia ngozi isiyo na kasoro.