Mgogoro mzito unaripotiwa ndani ya CHADEMA


Chama chama Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) Kimeingia katika wingu zito na kutishia kukisambaratisha chama hicho.

Chanzo cha Mgogoro ni nafasi za Ubunge wa Africa mashariki, Uchaguzi wa kanda ya Mashariki na Hali ya kifedha ndani ya chama.

Chanzo cha ndani ya CHADEMA kinasema kuwa mwenyekiti wa CHADEMA Ndugu Freeman Mbowe aliingia na majina mawili ndo akawaambia wayachague ambapo aliingia na Majina hayo ni Masha na Wenje hakukua na utaratibu sahihi wa kuwapata wagombea katika Bunge la Africa Mashariki.

Uchaguzi wa kumpata Viongozi ndani ya kanda ya Mashariki ulijaa kasoro nyingi ambapo wananchama wanaulinganisha na ule wa kanda ya Nyasa ambapo Ole Sosopi alitupwa nje ya kinyang'anyiro kwa kuwa mwenyekiti wa chama aliingia na Jina lake.

Idara ya fedha ndani ya CHADEMA haijakaa vizuri hivyo kuleta sintofahamu kwa wadhamini ambao wanataka ukaguzi wa fedha kupitia mkaguzi huru akague ili wajiridhishe wadhamini ndani ya CHADEMA wamekua wagumu kutoa fedha zao Hali ambayo inaisababishia chama ukata kwani Tajiri na Mdhamini mkubwa ndani ya CHADEMA ndugu Sabodo Alishajitoa na Kuungana na Rais Magufuli baada ya kuona Utendaji wake uliotukuka.