Uchunguzi: Tuhuma nzito TRA Njombe

WANANCHI mkoani Njombe wameleza mashaka yao kwa mamalaka ya Mapato TRA wilaya ya Njombe kutokana kutopewa lisiti za EFD wakati wa manunuzi ya huduma na bidhaa mbali mbali katika eneo hilo.

Wananchi hao kwa nyakati tofauti wakizungumza na Muungwana Blog wamedai kuwa wanapoulizia mashine hizo hujibiwa na wafanya biashara hao kuwa ni hawazijui mashine hizo na hawana majibu ambayo yalitafsiriwa na wananchi hao kuwa ni mipango ya ualaji kati ya TRA na wafanyabiashara hao.

Mmoja wa wananchi hao ambaye hakutaka kutajwa jina lake amesema kuwa alifika kwenye moja ya Hoteli Mkoani humo na kuhudumiwa bila ya kupewa lisiti za malipo zinazotokana na mfumo wa ulipaji kodi EFDs ambapo alilazimika kudai lisiti hiyo na kuambiwa kuwa hakuna na kwamba wao hawajui uwepo wa mashine hizo.

Mwengine alituonyesha ushahidi wa lisiti ambazo amerejeshewa baada ya kuhudumiwa ambazo sio za EFD.

“Nimeshangazwa kuona eti wafanya biashara wa iringa wanadai kuwa hawana mashine za EFD na kwamba wanadai kuwa hata watu TRA huwa wanakuja maenao hayo kupata huduma mbalimbali mfano hapo Hotelini nilipokula naambia TRA hufika na kula hapo lakini hakuna mashine za kukusanya mapato za EFDs.


Mwengene amesema kuwa yupo tayari kutupeleka ili kuthibitisha kuwa hakuna lisiti ya EFD wanazopewa baada ya huduma ilhali wanadai.


lisiti zinazotumika kwenye Hotel mbalimbali katika eneo la Njombe



Hata hivyo muungwana Blog ilizungumza na Meneja wa TRA wilaya ya Njombe kuueleza mtandao huu kuwa yeye hana Mamlaka ya kuzungumza na vyombo vya hanari hivyo tuzungumze na Meneja wa Mkoa wa Iringa.

Muungwana Blog ilizungumza na Meneja wa TRA Mkoa wa Iringa Jeseph Kalinga , ambaye amesema kuwa kuhusu suala hilo anasikia kwetu (mwandishi wa habari hizi)  na kwamba  ni vema watu wa eneo hilo wakaenda kwa Meneja wa TRA wilaya ya Njombe na kueleza malalamiko hayo ili yafanyiwe kazi na kwamba utakuwa ushahidi wa kuwawajibisha wafanya biashara wanaoepuka kutumia mashine hizo.

Hata hivyo Kalinga ameagiza wananchi kudai lisiti za EFD ili kuhakkisha kuwa wanalipa kodi kwa ajili ya maendeleo ya taifa.

“Naomba hao watu waende kwa Meneja TRA wilaya ya Njombe ili iwe rahisi kupata ushahidi wa wafanya biashara gani wanaokwepa kutumia mashine hizo” amesema Kalinga.


Mpya zaidi Nzee zaidi