VIDEO: Hii ndiyo hukumu ya kuua bila kukusudia

Wakili wa kujitegemea Jebra Kambole amezungumza na Muungwana Blog na kusema kuwa, Kwa mujibu wa kifungu namba 195, sura ya 16 kanuni za adhabu ndio kifungu kilichoelezea maana ya kesi ya kuua bila kukusudia na adhabu zake.

Katika  sheria  ya kuua  bila  kukusudia  (manslaughter)  kunatofautishwa  na  kuua  kwa  kukusudia (murder) kwenye kifungu hicho. Kuua  bila  kukusudia  ni  kuua ambako  muuaji  anatenda  kitendo hicho kinachopelekea  umauti  lakini bila dhamira, lengo au nia ya kukusudia kuua.

Wakati  kuua  kwa  kukusudia  ni  pale  mtu  anapotenda  tendo   ambalo  linapelekea  mauaji  ya  mtu   lakini  amefanya  hivyo  akiwa  amedhamiria   kuua.  Kwahiyo  haraka  utaona  kuwa  tofauti  kubwa  ya  kuua kwa  kukusudia  na  ile  ya  kuua  bila  kukusudia  ni  dhamira, nia au  lengo.

Je, utajuaje kuwa mtuhumiwa aliua bila kukusudia na zipi adhabu zake? 

TAZAMA FULL VIDEO HAPO CHINI

Mpya zaidi Nzee zaidi

Popular Items