Waziri Jafo azuia shule ya Ihunge kuwa chuo kikuu

Waziri wa Nchi,Ofisi ya Rais,TAMISEMI Selemani Jafo amewasisitiza viongozi wa mkoa wa Kagera kutokubadilisha malengo ya shule ya Ihungo kwa kuigeuza kuwa chuo kikuu baada ya kukamilika kwa ujenzi.

 Jafo ameyasema hayo alipokuwa akikagua maendeleo ya ujenzi wa shule hiyo inayojengwa upya baada ya hapo awali kukumbwa na tetemeko la ardhi.
Shule ya Ihungo inajengwa kisasa na  itakapokamilika itakuwa shule ya kipekee kwa kuwa na miundombinu ya kisasa hapa nchini.

Amesema Majengo ya shule hiyo kwasasa yanaweza kuwatamanisha baadhi ya viongozi kutaka kubadilisha shule hiyo hapo baadae kuwa chuo kikuu kitu ambacho amezuia jambo hilo.

Amesema amezuia ili vijana wa kidato cha tano na sita ili waweze kupata nafasi kusoma katika shule hiyo yenye mazingira mazuri.

Baada ya ukaguzi wa shule hiyo,Waziri Jafo alielekea na ukaguzi wa shule nyingine ya Nyakato inayojengwa na Suma JKT na kuridhishwa na maendeleo ya ujenzi.