Ndege yaanguka na kuua watu watano


Watu watano wamekufa baada ya ndege nodogo kuanguka katika eneo la Santa Ana katika jimbo la California.

Inadaiwa rubani wa ndege hiyo alitoa taarifa ya hali  ya hatari kabla ya ndege hiyo kuanguka na kusababisha vifo hivyo.

Katika ajali hiyo hakukuwa na mtu aliyenusurika na tayari vyombo vinavyohusika na usafiri wa anga vimeanza uchunguzi kubaini chanzo cha ajali hiyo.

Ndege hiyo ilianguka katika eneo la maduka katika mji huo na kuangukia moja kati ya gari lililokuwa limeegeshwa.
Mpya zaidi Nzee zaidi

Popular Items

Ujuwe Ugonjwa wa Busha