Serikali yawataka wakaguzi kushirikiana na waalimu


Naibu waziri wa elimu mafunzo ya ufundi William Olle  Nasha amewataka wadau wa sekta ya  elimu  wakiwemo  wadhibiti na wakaguzi kuacha kutumia  changamoto zilizopo kuwabebesha  walimu mzigo wa  lawama  badala yake  wasaidiane  nao  kuzitatua.

Akizungumza na wadhibiti wa viwango vya elimu wa mkoa ya kanda  ya kaskazin Olle Nasha amesema baadhi  ya  watendaji  wa  sekta hiyo wakiwemo wakaguzi wamekuwa wakikimbilia kukagua  mapungufu tu na kuwaachia walimu kana  kwamba  wao  hawahusiki  na kwamba wanaofanya hivyo watawajibishwa.

Mdhibiti wa ubora wa shule kutoka wizara ya elimu Agusta  Mpokela  pamoja  na kukiri kuwepo kwa changamoto  amesema  zinaendelea kushughulikiwa na  kupungua  baada  ya  kuanza  kutumka  kwa  mfumo  mpya  elimu.

Olle Nasha pia ametembelea na kukagua karakana ya chuo cha  ufundi Arusha na kueleza kuwa  serikali  inaendelea  kuviboresha  na kuviimarisha kwa kuweka  vifaa , mashine  na zana za kisasa  za  kufundishia.

Baadhi ya watendaji wa vyuo vya ufundi  wamesema pamoja  na  serikali  kutumia  mabilioni ya fedhakuwekeza katika vifaa  vya  kisasa  kuna  changamoto  kubwa  ya  uwezo mdogo  wa wanafunzi  wanajiunga  na  vyuo  hivyo. 
Mpya zaidi Nzee zaidi

Popular Items

Ujuwe Ugonjwa wa Busha