Korea Kaskazini yakubali kufunga kituo cha Nyuklia, yaipa Marekani masharti


Kiongozi wa Korea Kaskazini Kim Jong Un ameahidi kukiteketeza kituo Kikuu cha nyuklia cha  Tongchang-ri na badala yake kuanzisha kituo cha kurushia mizinga katika eneo hilo baada ya mazungumzo na Rais wa Korea Kusini Moon Jae-In.

Akiongea na waandishi wa habari katika mkutano uliowakutanisha na  kiongozi wa Korea kaskazini, rais wa Korea Kusini Moon Jae-In amesema baada ya mkutano uliofanyika Pyongyang ,kiongozi wa Korea Kaskazini Kim Hong Un amekubali kukifunga kinu cha Tongchang-ri na kufungua kituo cha mizinga kwa usimamizi wa nchi washirika.

Hata hivyo kiongozi wa Korea Kaskazini amesema atakifunga kinu cha nyuklia cha Nyongbyong iwapo Marekani itayafanyia kazi makubaliano waliyowekeana.
Mpya zaidi Nzee zaidi

Popular Items