UPDATES: Wazungu wawili wamteka MO Dewji



Mfanyabiashara Mo Dewji

Mfanyabishara maarufu nchini ambaye pia ni muwekezaji wa klabu ya Simba, Mohammed Dewji (MO) amedaiwa kutekwa na watu wasiojulikana, saa 11 Alfajiri ya leo.

Kamanda wa Polisi Kanda Maalum Lazaro Mambosasa amesema kwamba wameweka vizuizi kuhakikisha hakuna mtu anayetoka, ili watekaji wasitoke nje ya nchi, na kwamba waliohusika kwenye tukio la kumteka Mo Dewij ni raia wawili wa kigeni (wazungu).

Mambosasa amesema kuwa tayari wameweka vizuizi kuhakikisha hakuna anayetoka, ili watekaji wasitoke nje ya nchi.

Tukio hilo limetokea katika ‘Gym’ ya Colosseum iliyopo Oysterbay jijini Dar es salaam ambapo mfanyabiashara huyo alipokuwa akiingia kufanya mazoezi.