Mfanyabiashara Mo Dewji
Kamanda wa Polisi Kanda Maalum Lazaro Mambosasa amesema kwamba wameweka vizuizi kuhakikisha hakuna mtu anayetoka, ili watekaji wasitoke nje ya nchi, na kwamba waliohusika kwenye tukio la kumteka Mo Dewij ni raia wawili wa kigeni (wazungu).
Mambosasa amesema kuwa tayari wameweka vizuizi kuhakikisha hakuna anayetoka, ili watekaji wasitoke nje ya nchi.
Tukio hilo limetokea katika ‘Gym’ ya Colosseum iliyopo Oysterbay jijini Dar es salaam ambapo mfanyabiashara huyo alipokuwa akiingia kufanya mazoezi.