Fissoo amempongeza msanii huyo jijini Dar es Salaam alipokutana naye na kuzungumzia masuala mbalimbali ya Maendeleo ya Tasnia ya Filamu na Michezo ya Kuigiza nchini.
Aidha Fissoo alimkumbusha Monalisa na Wadau wote wa Sekta ya Filamu na uigizaji umuhimu wa kuendelea kutoa taswira chanya katika jamii na kuwa mfano wa kuigwa kwenye jamii.