Mataluma: Nataka nimuoe Gigy Money nikimpata ntatulia kabisa



Baada ya kuyumbishwa kwenye mausiano kwa muda mrefu na mama watoto wake Msanii Mataluma aliyewahi kufanya vizuri na ngoma zake kama ‘Mama Mubaya’ ‘Kariakoo’ wakati huo Mataluma  kuvunja ukimya na kusema nibora amuoe mwanamke aliyopo kwenye tasnia yake Gigy Money.

Gigy amesema kuwa anataka kumuoa msanii huyo ambaye pia ni video vixen huku akisema kuwa hajui kama atakubali kwasababu anaamini msichana huyo atakuwa na mapenzi ya dhati.

"Yaani Gigy money yule mtoto yule kama anatulia mi namchukua, Gigy Money nataka nimuoe sijawahi sikia harusi yake naamini mimi yule Gigy money nikimpata ntatulia kabisa kwasababu sio leo ni siku nyingi lakini unakuta kuna watu washarukia," amesema Mataluma katika Mahojiano yake na EATV.

"Gigy wale hawakupendi mume wako nipo nataka nikuoe sasa sijui mwenyewe kama atakuwa tayari au vipi au najisemesha, Ukweli ndio huo Gigy i love you so much napata shida na Gigy ana mapenzi ya dhati ila hajapata mtu."