https://monetag.com/?ref_id=TTIb BREAKING: Rais George Bush afariki Dunia | Muungwana BLOG

BREAKING: Rais George Bush afariki Dunia

George H.W. Bush

Rais wa zamani wa Marekani George H.W. Bush amefariki dunia akiwa na umri wa miaka 94 huko mjini Houston, msemaji wake Jim McGrath amethibitisha kifo chake.

Rais huyo wa zamani wa Marekani aliongoza kwa awamu moja tu akiingia madarakani mwaka 1989 na kuondoka 1993 hivyo kubaki kama Rais pekee aliyeiongoza Marekani kwa awamu moja.