Kundi la Navy Kenzo mbioni kuachia albamu ya pili


Kundi la muziki wa Bongo Fleva, Navy Kenzo lipo katika mpango ya kutoa albamu yao ya pili tangu kuanza kufanya vizuri kwenye muziki.

Utakumbuka December 2016 ndipo Navy Kenzo walitoa albamu yao ya kwanza inayokwenda kwa jina la Above In A Minute (AIM).
Albamu yao ya kwanza, Above In A Minute (AIM).
Tangu walipotoa albamu hiyo ya kwanza Navy Kenzo wametoa nyimbo mbili ambazo ni Fella na Katika waliyomshirikisha Diamond Platnumz. Hivyo albamu hiyo moya itakuwa na utitiri wa nyimbo nyingi mpya.
Mpya zaidi Nzee zaidi