Timu nane kuingia dimbani Leo Ligi ya Wanawake


Viwanja vinne Leo vumbi litatimka kufuatia michuano ya Ligi ya Wanawake Tanzania maarufu kama Serengeti Lite Women's Premier League kuendelea timu nane kushuka Uwanjani kumtafuta mbabe wa pointi tatu.

Ligi hiyo ambayo bingwa mtetezi ni JKT Queens, Evergreen Queens kazini leo uwanja wa Karume kumenyana na Baobab Princess, JKT Queens mzigoni kumenyana na Sisterz FC uwanja wa Mej.Gen.Isamuhyo.

Marsh Queens watachuana na Mlandizi Queens uwanja wa Nyamagana na Mapinduzi Queens mzigoni leo uwanja wa Sabasaba dhidi ya Simba Queens, mechi zote hizi zitaanza saa 10:00 jioni.
Mpya zaidi Nzee zaidi

Popular Items

Ujuwe Ugonjwa wa Busha

Kilimo cha Bamia