Mwaka umetimia kuachana kwa Diamond na Zari


Ikiwa leo ni siku ya Wapendano (Valentine’s Day), tarehe kama ya leo mwaka jana ndipo
Zari The Bosslady alitangaza kuachana na Diamond.

Zari alitangaza kuvunja rasmi mahusiano yake na Diamond Platnumz akiwa nchini Kenya kwa
ajili ya event yake ‘The Colour Purple’ itakayofanyika weekend hii Uhuru Gardens.

Zari alisema ameachana na Diamond kutokana alikuwa akimvunjia utu wake kwenye mitandao
ya kijamii kwa kujihusisha kwenye mahusiano ya kimapenzi na wanawake mbalimbali.

Baada ya kuachana kwao, Zari hajaonekana tena kwenye mahusiano na mtu mwingine, wakati
Diamond akiwa na mrembo kutoka nchini Kenya, Tanasha ambaye pia mtangazaji wa redio.