Rwanda kuanzisha kiwanda chake cha kwanza cha utenegenezaji wa simu za kisasa

Wizara ya sayansi na teknolojia , mawasiliano chini ya uongozi wa Paula Ingabire nchini Rwanda amesema kwamba tayari mazungumzo yameanza na sekta binafsi kwa lengo la  kuanzisha  kiwanda cha kwanza cha utengenezaji wa simu za kisasa.

Kulingana na taarifa zilizotolewa na  vyombo vya habari nchini Rwanda, kiwanda hicho  itakuwa ni hatua kubwa  katika sekta ya teknolojia na mawasiliano katika ulimwengu wa kisasa ambao umekuwa kama kjiji kimoja.