Baba Diamond afunguka ishu ya kusainiwa WCB


Baba Diamond, Abdul Juma amefunguka ishu ya kusainiwa WCB kwenye lebo ya mtoto wake Diamond Platnumz.

Mzee juma amesema kuwa kwenye mambo ya kutafuta riziki anaweza akaajiriwa na mwanae huku akisema ukitaka cha uvunguni sharti uiname.

"Unajua kitu kama hicho hapo, ushajua kama kuna mapato fulani au kitu fulani kama vitu vyenywe vinakuwa sio vizito si unatafuta riziki bwana mtaka cha uvunguni sharti uiname," alisema Mzee Juma.