Watumishi NAOT waaswa kuzingatia Maadili


Watumishi wa Ofisi ya Taifa ya Ukaguzi (NAOT) wameaswa kuziungatia Maadili wakati wote wanapotekeleza majukumu yao ili kuendana na dhamira ya Serikali kufikia maendeleo endelevu na uchumi wa kati.

Akizungumza wakati akizindua Baraza jipya la wafanyakazi wa Ofisi hiyo leo Jijini Dodoma Naibu Katibu mkuu Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Utumishi wa Umma na Utawala Bora Dkt. Francis Michael amesema watumishi wote wa Ofisi hiyo wanapaswa kuhakikisha kuwa wanazingatia sharia kanuni na taratibu za utumishi wa umma ili kuleta tija katika majukumu wanayotekeleza.

“Sitarajii Wakaguzi wetu Wakawa miongoni mwa watumishi watakaokumbwa na kashfa za namna yoyote hivyo niwaase kujiepusha na vitendo vya utovu wa nidhamu,kudai na kupokea rushwa” Alisisitiza Dkt. Michael

Akifafanua amesema kuwa hatma ya makosa hayo ni kupoteza ajira na kufikishwa katika vyombo vya sheria ikiwemo mahakama ili sharia iweze kuchukua mkondo wake hali inayoweza kupelekea mhusika kufungwa jela.

Aidha, aliwataka wajumbe wa Baraza hilo kutumia fursa za Dodoma kuwa makao makuu ya Serikali kujiletea maendeleo kwa kuwekeza katika sekta mbalimbali ikiwemo ardhi.

Kwa upande wake Mdhibiti na Mkaguzi mkuu wa Serikali Prof. Mussa Assad amesema kuwa Ofisi hiyo imekuwa ikitekeleza majukumu yake kwa weledi ili kutimiza lengo la kuanzishwa kwake ikiwemo kuhakikisha kuwa ripoti ya ukaguzi inatolewa kama inavyotakiwa kila ifikapo mwezi machi.
Mpya zaidi Nzee zaidi