Indonesia yakumbwa na tetemeko la ardhi

Tetemeko la nchi lenye ukubwa wa 6.4 limeikumba nchi ya  Indonesia.

Kulingana na Mamlaka ya Hali ya Hewa ya Indonesia tetemeko hilo limefikia kina cha kilomita 216 kusini mashariki mwa Malku nchini humo.

UNHCR na Kituo cha Tsunami cha Pasifiki hawakutoa tahadhari ya tsunami baada ya tetemeko la ardhi.

Kulingana na matokeo ya awali, hakuna mtu aliyekufa au kujeruhiwa katika tetemeko la hilo.

Nchini Indonesia, Septemba 28, 2018, tetemeko la ardhi lenye ukubwa wa 7.5-lilitokea katika Ghuba la Palu kwenye Kisiwa cha Sulawesi ikifuatiwa na tsunami iliyoathiri mikoa ya Donggala, Palu na Sigi.

Watu zaidi ya elfu nne walipoteza maisha.