Na Ferdinand Shayo,Arusha.
Wanafunzi waliohitimu kidato cha sita katika shule mbalimbali wanatarajia kupatiwa mafunzo ya ujasiriamali yatakayowawezesha kutambua fursa zilizowazunguka pamoja na kujiajiri ili kupunguza tatizo la ajira miongoni mwa vijana.
Mkuu wa Idara ya Ushauri katika Chuo cha Uhasibu Arusha Pamela Chogo alisema kuwa wameamua kutoa mafunzo kutokana changamoto wanazoziona kwa wanafunzi wa vyuo mbalimbali pindi wanapohitimu masomo yao.
Alisema mafunzo hayo ya ujasiriamali yatawasaidia kufanya maamuzi ya kijana katika maisha na kuweza kujitambua ili waweze kujiajiri kutokana na tatizo La soko ajira lililopo nchini.
Mafunzo hayo ni ya muda wa wiki sita nayataanza tarehe 10 mwezi wa sita yakilenga kufundisha elimu mbali mbali ya ujasiriamali,namna ya kujitambua pamoja na jinsi ya kuweza kuajiriwa.
"Ili kuhakikisha tunatoa elimu hiyo kwa undani zaidi tutawaalika wadau wa wataalamu wa SIDO kutoa elimu ya ujasiriamali pamoja na wataakamu wa mikoani kwaajili ya kutoa elimu ya mikopo wataalamu wa Afya" alisema Pamela Kichogo.
Adha alisema katika kutoa elimu ya Afya itawasaidia vijana katika Afya ya uzazi kwani vijana wengi hawaelewi Afya ya uzazi hivyo ulazimika kutafuta taarifa hizo kwenye mitandao ambayo haina ukweli wa kile wanachokihitaji.
Mbali na hilo watatoa elimu ya kujisimamia na jinsi ya kujilinda kama kijana hususani kwa wale waliohitimu elimu ya sekondari kwani vijana wengine hawawezi kujilinda huku wengi wao wakiingia katika makundi ya mitaani na kufanya uhalifu.
Hata hivyo vijana wametakiwa kuachana na dhana ya kubweteka na kulalamika lika siku kuwa kahuna ajila huku wa kitakiwa kuzingatia kuwa Tanzania ya Viwanda inawezekana na waanzilishi wa viwanda hivyo ni wao na siwengine.