Wizara ya Madini na Wizara ya Fedha na Mipango zimesaini makubaliano ya mkakati wa ukusanyaji wa maduhuli kwa mwaka wa fedha 2019/2020 ya Tsh. Bilioni 475.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Madini Simon Msanjila ndiye amesaini makubaliano ya mkakati wa ukusanyaji wa maduhuli kwa mwaka wa fedha 2019/2020 kati ya Wizara ya Madini na Wizara ya Fedha na Mipango jijini Dodoma hapo jana.

