Maajabu: Mume akwama kwa mkewe


Wanandoa nchini Marekani walipelekwa hospitalini katika hali mbaya, baada mume kukwama (kunasa) kwa mkewe wakati wakishiriki tendo la ndoa.

Wanandoa hao wanasemekana kuwa walikuwa wakishiriki ngono, japo bado haijafamika ni ngono ya aina gani.

Tom na mkewe Janis Morrison, wanandoa kutoka mji wa Greensboro, Alabama wanaripotiwa kupigia simu namba ya dharura 911 saa nne usiku, wakiomba msaada wa ambulensi ya kuwapeleka hospitalini.

Samantha Irving ambaye alipokea simu hiyo, hata hivyo, alisema aliona kama ulikuwa mzaha alipoambiwa tatizo.

Madaktari hao walisema kuwa waliwapata wawili hao wakiwa uchi kitandani, huku damu ikiwa imetapakaa. Walikimbizwa katika hospitali ya karibu, ambapo walihudumiwa na kutenganishwa.