Misri yatupwa nje AFCON 2019

Misri wanatupwa nje ya mashindano kwa bao 1-0 huku Afrika Kusini wakisonga mbele kwenye hatua ya robo fainali ya AFCON 2019.

Bao pekee la Afrika Kusini limefungwa na Thembinkosi Lorch mnamo dakika ya 85 ya kipindi cha pili.

Misri sasa wanaungana na timu za Cameroon ambao nao leo wamekubali kichapo cha mabao 3-2 kutoka kwa miamba Nigeria.