F R Kelly anyimwa dhamana | Muungwana BLOG

R Kelly anyimwa dhamana

Mwanamuziki nyota wa R and B R.Kelly baada ya kuzuiliwa kwa mara nyingine akituhumiwa kuuza wanawake wenye umri mdogo kwa ajili ya ngono  atarajiwa kufikishwa mahakamani Jumanne Julai 23 kwa aijli ya kusikilizwa kama ana haki ya kupewa dhamana.

Kutokana na tuhuma zinazomkabilia msanii , mahakama ya Chicago imemnyima dhamana .

Mwanamuziki huyo mwenye umri wa miaka 51  amekumbwa na tuhuma kemkem za unyanyasaji wa ngono.

Kwa upande wake msanii huyo anadai kuwa ni njama dhidi yake.