Aliyekuwa Mwandishi wa Azam Media Salim Mhando asomewa hitma


Watu umejitokeza nyumbani kwa marehemu, Salim Mhando kwa ajili ya kumsomea hitma.

Salim ni miongoni mwa wafayakazi watano wa Azam Media waliofariki katika ajali iliyotokea eneo la Shelui, mkoani Singida, iliyohusisha magari mawili yaliyogongana uso kwa uso.

Wafanyakazi hao wa Azam TV walikuwa njiani kwenda kurusha matangazo mbashara ya uzinduzi wa Hifadhi ya Taifa ya Burigi-Chato.