Askofu Dk. Fredrick Shoo achaguliwa kuwa Mkuu wa Kanisa KKKT


Mkuu wa Kanisa la  Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), Dkt.  Frederick Shoo amechaguliwa tena kuliongoza Kanisa kwa kipindi cha Miaka mingine minne.

Dk Frederick Shoo amepata kura 144 dhidi ya 74 za mpinzani wake. Atafuata nyayo za wakuu wa kanisa hilo waliomtangulia walioliongoza kwa vipindi viwili vya miaka minne.

Ametangazwa kuwa mshindi usiku wa kuamkia leo baada ya kumalizika kwa uchaguzi uliofanyika mjini Arusha na kutawaliwa na kila aina ya upinzani.


Mpya zaidi Nzee zaidi

Popular Items