Chelsea ya Lampard ngoma nzito ligi kuu, washindwa kutamba kwa madogo


Klabu ya soka ya Chelsea imeshindwa kufurukuta katika uwanja wake wa nyumbani Stamford Bridge baada ya kutoka sare ya kufungana mabao 2-2 dhidi ya Sheffield United kwenye mchezo wa ligi kuu ya Uingereza.

Chelsea ndio walikuwa wakwanza kupata mabao yao katika kipindi cha kwanza kupitia kwa Tammy Abraham (dakika ya 19 na 43).

Sheffied United walizawazisha kupitia kwa Callum Robinson aliyefunga dakika ya 46 na Kurt Zouma ambaye alijifunga dakika ya 89 ya mchezo huo.

Huu ni mchezo wa pili kwa Chelsea kutoka sare msimu huu huku akiwa tayari amepoteza mchezo mmoja na kushinda mmoja.