Muimbaji wa muziki wa injili nchini Goodluck Gozbert amefungukza kuwa hakuandika wimbo wa "Nibadilishe" kwa ajili ya watu waliookoka.
Kiongea kwenye kipindi cha Bongo Fleva cha Clouds FM, Gozbert amesema, “SikuandikaNibadilidshe kwa ajili ya watu waliookoka.”
“Wakati naandikaNibadilishesikufanya kwa ajili ya watu ambao wapo tayari kwenda mbinguni, bali nilifanya kwa ajili ya watu ambao wanajua kila kitu kuhusu dini yake na wanajua kuhusu Mungu na kuna vitu wanashindwa kuvifanya vya kiimani na hawajui kwanini vinawashinda,” ameongeza.
Msanii huyo amesema hayo baada ya watu wengi wamekuwa wakizungumza kuwa wimbo huo haujakaa ki-gospel.