https://monetag.com/?ref_id=TTIb Liverpool sasa ina mataji mengi makubwa kuliko Man United | Muungwana BLOG

Liverpool sasa ina mataji mengi makubwa kuliko Man United


Klabu ya Liverpool imepiku mahasimu wao wa jadi Manchester United kwa mataji na sasa ndiyo timu iliyopata ufanisi mkubwa nchini Uingereza baada ya kubeba taji la UEFA Super Cup Jumatano usiku.

Mabingwa wa Klabu Bingwa Ulaya Liverpool, ambao wanafahamika kwa jina la utani kama 'The Reds', waliwachapa washindi wa Ligi ya Ulaya Chelsea kwa njia ya penalti 5-4 na kufikisha mataji 46 makubwa.

Mataji ya Liverpool yanajumuisha 18 ya Ligi Kuu, saba ya Kombe la FA, manane ya League Cup, sita ya Klabu Bingwa Ulaya, matatu ya Ligi ya Uropa na manne ya Uefa Super Cup.