Mwanamke avuka mto wenye urefu wa Mita 350 kwa kamba bila kinga


Mwigizaji wa kutembea kwenye kamba Tatiana-Mosio Bongonga kutoka Ufaransa amevuka mto Vltava kwa kutumia kamba yenye urefu wa mita 350 huko Prague, mji mkuu wa Jamhuri ya Czech.

Alivuka mto bila kinga yoyote inayoonekana, akitumia kiimo cha kusawazisha chenye uzito wa kilo 12. Safari nzima ilimchukua kama dakika 40.

Mwanasarakasi huyo alikaa juu ya kamba mara kadhaa alipokuwa akitembea na hata kulala na pia kujishikilia kwa nyayo zake zilizoinama kutoka kwenye kamba. Maelfu ya watu walikuwa wakitazama na kupiga makofi.