Man United hali tete ligi kuu, yabanwa na Southampton ugenini


Klabu ya soka ya Manchester United imeendelea kujikuta ikiwa na wakati mgumu ndani ya ligi kuu nchini Uingereza msimu huu.

Timu hiyo Jumamosi hii imetoka sare ya kufungana bao 1-1 dhidi ya Southampton ambao walikuwa wenyeji wa mchezo huo.

Man United ndio walikuwa wakwanza kupata goli dakika ya 10 kupitia kwa Daniel James, hata hivyo Jannik Vestergaard dakika ya 58.

Wakati huo huo mchezaji wa Southampton Kevin Danso alitolewa nje kwa kadi nyekundu dakika ya 73 baada ya kuwa na kadi mbili za njano.

Kwa sasa United inashika nafasi ya saba kwenye msimamo wa ligi kuu ikiwa na alama tano na tayari imeshacheza michezo minne wakati Manchester City akiongoza akiwa na alama 10 akiwa amecheza michezo minne.