Msanii Kanye West na waumini wake wafanya ibada ya kipekee


Rapa kutokea Marekani, KanyeWest juzi aliungana na baadhi ya waumini wake na kufanya shoo barabarani mjini California huku wengine wakiendelea na ibada kanisani.

Msanii huyo ambaye mapema mwaka huu alitangaza kufungua kanisa lake na alifanikiwa kupata waumini wengi ambapo kila Jumapili amekuwa akiungana nao na kufanya ibada.

Lakini Jumapili ya wiki iliopita ibada ilikuwa ya aina yake ambapo baadhi ya waumini waliungana na msanii huyo na kufanya shoo barabarani huku wengine wakiendelea kufanya ibada kanisani.

Hata hivyo baada ya kumaliza kufanya ibada hiyo waliendelea kupata burudani ya msanii huyo kwa kutumia runinga huku wakiwa kanisani.