Mwanamitindo Bongo Ben Breaker atajwa kuwania tuzo nyingine Ghana


Mwaka 2019 huenda ukawa ni waneema kubwa kwa mwanamitindo wa kiume hapa Bongo, Ben Breaker - Baada ya kuchaguliwa kuwania tuzo za Star QT za Afrika Kusini, amefanikiwa kupata dili jingine nchini Ghana.

Breaker amechaguliwa kuwania tuzo kubwa za nchini humo zinazofahamika kama "Odartey Style and Fashion Awards".

Katika tuzo hizo Ben amechaguliwa kuwania katika vipengele viwili ambavyo ni ambavyo ni Best Icon na People's Choice.

Tuzo hizo zinatarajiwa kufanyika mjini Accra, February ya mwaka 2020.