Faiza Ally ajibu mapigo baada ya mzazi mwenzake Sugu kuoa, "Hope you will treat me well tonight"


kuna msemo unasema, "Ukisema cha nini basi mwenzako anajiuliza atakipata lini" hilo limejidhihirisha Jumamosi hii baada ya mbunge wa Mbeya Mjini, Joseph Mbilinyi "Sugu" kufunga ndoa na mpenzi wake Happiness Msonga.

Wawili hao wamefunga ndoa hiyo katika kanisa la Katoliki Ruanda Parokia ya Roho Mtakatifu.

Hata hivyo muda mfupi baada ya ndoa hiyo kupita mzazi mwenzake na Sugu, Faiza Ally ameandika ujumbe kupitia mtandao wa Instagram ambao baadhi ya mashabiki wa ubuyu wa mitandaoni wamechukulia ni kama amejibu mapigo.

Kupitia mtandao huo, Faiza ameandika, "Hello beautiful ☺️☺️ Hope you will treat me well tonight 😉👄🥂."