Ninaamini Simba SC haiwajengi tu wapinzani - MO Dewji


Mwenyekiti wa Bondi ya Wakurugenzi, Simba SC Mohammed Dewji amesema kufanya vizuri kwa timu hiyo kunapelekea na timu nyingine nchini kuwa na ujasiri zaidi pindi wanapocheza na vilabu vingine vya nje.

Amesema hayo katika na mahojiano na BBC Radio na kueleza huo ndio mwanzo wa wachezaji wa ndani kwenda kucheza soka la kulipwa Ulaya.

"Ninaamini Simba haiwajengi tu wapinzani, pia inazipa ujasiri timu zingine, ukiwa na timu nzuri za ndani pia unakuwa na timu nzuri ya Taifa na hapo ndio wachezaji wataweza kwenda kucheza Ulaya na sehemu nyingine" alisema MO Dewji.