https://monetag.com/?ref_id=TTIb SADC yapania kuimarisha miundombinu ya usafirishaji | Muungwana BLOG

SADC yapania kuimarisha miundombinu ya usafirishaji


Sekretarieti ya Miundombinu ya Jumuiya ya Maendeleo ya Nchi za Kusini Mwa Afrika (SADC) inajikita katika kuimarisha na kuboresha miundombinu ya usafirishaji kwa kufanya ukarabari na kuhuisha sekta hiyo hususani sekta ya Bandari, Reli na Anga.

Akizungumza na Waandishi wa Habari Jijini Dar es Salaam, Mkurugenzi wa Wa Sekritarieti ya SADC Miundombinu, Bi.Rosemary Makoena amesema kuwa hakuna Maendeleo pasipokuwa na uimarishwaji wa sekta hiyo, ili kuhakikisha kuwa nchi wanachama wanaunganishwa na sekta hiyo kufanya biashara katika ukanda wao.

Ameongeza kuwa Miundombinu unayopigiwa chapuo kwenye utekelezaji wa Mpango Mkakati wa Miaka 5 ni pamoja na Miundombinu ya Usafirishaji ambayo imebeba dhamira kubwa kwenye kuimarisha mawasiliano ya kibiashara baina ya nchi wanachama.

“Katika Mpango Mkakati wa 2015-2020 kwa nchi wanachama wa SADC tunaangalia zaidi kwenye utekelezaji na uangalizi wa miradi ya uimarishwaji wa miundombinu ya kusafirisha bidhaa.Mpango mkakati huo unalenga kuimarisha Sera mbalimbali ikiwemo ile ya uendelezwaji na ukarabati wa Bandari (SADC Corridors of 2008) ya ukanda wetu wa kusini mwa Afrika”, Amesema Makoena.

Aidha, mpango huo wa SADC unalenga zaidi kwenye kusaini, kutekeleza na kuendeleza Sheria itakayozileta pamoja nchi wanachama katika kuendeleza sehemu za lango la usafirishaji wa majini. Hii itawezesha wananchi kwenye nchi hizo kufanya biashara kwa urahisi bila vikwazo vyovyote.

Akisisitiza jambo hilo amasema kuwa mpango huo unaendana na makubaliano ya wanachama walioko katika lango ya bandari mbalimbali zilizoko katika ukanda huo wa kusisni mwa Afrika. Ikianzia bandari ya Mtwara, Dar es Salaam, Trans-Kalahari, Central Beira na Nacala ambapo wanachama wataweke kanuni kulingana na makubaliano yao ya usafirishaji yalifanyika chini ya Memorandum of Unederstanding For South-North amasema Makoena.

Alisema kuwa katika kuimarisha sekta hiyo ya usafirishaji wa majini, nchi wanachama walioko kwenye lango la bandari wanaweka kanuni, lengo, katiba na namna ya kuungana katika kuendeleza miradi ya ujenzi na ukarabati wa bandari hizo, ili kuboresha na kuhakikishi zinakuwa imara zaidi kwa kupokea mzigo ya kutosha.

“Katika kutekeleza na kuhakikisha kuwa sekta hii inaimarika azma kubwa tuliyonayo sisi kama Sekritarieti ya Miundombinu ni kuboresha na kuhuisha sekta hii ili iweze kufanya kazi kwa ufanisi na uhakika zaidi. Sekritarieti inaendelea na mpango mkakati wa mwaka 2012-2021 na kuungwa mkono na Jumuiya ya Ulaya-EU ambao wako tayari kusaidia kuimarisha miundombinu katika nchi wanachama wa SADC”, Amesema Makoena.

Katika Mpango mkakati huo Sekritarieti ya Miundombinu inalenga zaidi katika kuimarisha na kuweka kanuni tisa (9) za pamoja kwa wanachama ikiwemo Udhibiti wa Uendeshaji wa magari ya mizigo barabarani, viwango na vipimo vya magari ya mizigo na mizani ya kupima magari yote, kwani kanuni hizo ni muhimu kwa usalama wa barabara na bidhaa.

Pia, Machi mwaka 2018 SADC ialisaini makubaliano ya Sheria ya usafirishaji wa kuvuka mipaka miongoni mwa nchi wanachama inayojulikana kama Cross-Border Road Transporter-Regulator Forum (CBRT-RF). Ambayo inafanyakazi pamoja na Transport and Transit Facilitation Program (TTFP) yenye kazi ya kusimamia mambo ya usafirishaji yote hayo ni kuhakikisha Sekta ya usafirishaji inakuwa imara katika Jumuiya hiyo.

Makoena aliongeza na kusema kuwa sekta ya usafirishaji kwa upande wa Anga inaimarishwa ili kuwezesha kuwepo na ndege kubwa za mizigo katika ukanda huo wa kusini mwa afrika. Kwani usafiri wa anga ni moja wapo ya kichocheo muhimu katika kutekeleza ujenzi wa viwanda.

Hivyo, Sekritarieti ya Miundombinu inatekeleza hilo kwa kuanzisha Taasisi ya masuala ya usalama wa usafiri wa Anga (SADC Aviation Safety Organization,SASO) inayoshughilikia masuala ya usafiri wa anga katika nchi wanachama wa Jumuiya hiyo.

Pamoja na hayo, SADC miundombinu inaendelea na utekelezaji wa ukarabati na ujenzi wa Reli katika Nchi wanachama ili kuimarisha na kulinda usalama wa barabara, kwani mizigo mizito itakuwa inasafarishwa kwa njia ya treni na kuepuka uharibu wa barabara.

Akimalizaia Makoena alisema kuwa katika sekta ya Nishati SADC inajivunia utekelezwaji wa Mradi Mkubwa wa Ujenzi wa Bwawa la Umeme la Mto Rufiji nchini Tanzania,ambapo wanachama wa SADc watafaidika na umeme huo.

“Tunajivunia mradi huu, siyo SADC tu haya Jumuiya ya Afrika Mashariki-EAC, na tunakubaliana na kumuunga mkono kwa uongozi na mafanikio makubwa kwa Rais wa Sasa wa Tanzania katika utekelezaji wa mradi huo, tunahitaji kufanikisha hili kwa sababu tunahitaji Miundombinu hii. Amesema Makoena