Serikali yataifisha Pamba iliyokuwa ikisafirishwa kimagendo


Baada ya kukamatwa kwa tani 20 za pamba iliyokuwa ikisafirishwa kimagendo, Mkuu wa Wilaya ya Bariadi, Festo Kiswaga na kamati yake ya ulinzi na usalama wametaifisha pamba hiyo na kuiuza kwa kiwanda cha Alliance Ginneries na fedha iliyopatikana Shilingi 20 milioni imetumika kununua vifaa vya ujenzi Shule ya Sekondari Simiyu.